Add parallel Print Page Options

Petro Atambua Yesu ni Nani

(Mt 16:13-20; Lk 9:18-21)

27 Yesu na wanafunzi wake walikwenda kwenye vijiji vinavyozunguka Kaisaria Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi wake, “Watu wanasema mimi ni nani?”

28 Nao wakamjibu, “Yohana Mbatizaji. Wengine husema wewe ni Eliya. Na wengine husema wewe ni mmoja wa manabii.”

29 Kisha akawauliza wao, “Na ninyi; Je! Mnasema mimi ni nani?”

Petro akamjibu, “Wewe ni masihi.”

Read full chapter