Add parallel Print Page Options

Yesu Atakaporudi Tena

(Mt 24:29-51; Lk 21:25-36; 19:12-13,40)

24 Lakini katika siku hizo, baada ya kipindi cha dhiki,

‘Jua litatiwa giza,
    mwezi hautatoa mwanga,
25 nyota zitaanguka kutoka angani,
    na mbingu yote itatikisika.’[a]

26 Ndipo watu watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na nguvu kubwa na utukufu. 27 Baada ya hapo Mwana wa Adamu atawatuma malaika, na atawakusanya wateule wake kutoka kila upande wa dunia.

28 Jifunzeni somo hili kutoka katika mti wa mtini: Matawi yake yanaponyauka na kubeba majani, unajua kwamba kiangazi kimekaribia. 29 Vivyo hivyo, unapoona mambo haya yanaanza kutokea unajua kwamba muda umekaribia na umeshafika mlangoni. 30 Ninawaambieni ukweli: Kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo haya yote hayajatokea. 31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Read full chapter

Footnotes

  1. 13:24-25 Tazama Isa 13:10; 34:4.